Sehemu Ya (154) : Hali Halisi Ilivyo Kwenye Mahusiano Siku Hizi.. Unaweza Jifunza Kitu Hapa.
mke, mkewe akakataa,
akamwambia baba yake akaambiwa na babaake tulia mwanangu ndoa zina mengi! akawa
kila siku analalamika kwa babaake, mwisho babaake akamwambia basi ntakusaidia.
Itabidi ujifanye unaumwa sana hoi hujiwezi halafu nitakuonyesha jawabu!
Basi kijana akajifanya
anaumwa mzee akaitisha kikao cha ndugu wote pande Mbili Mzee akaanza kueleza
jamani kijana wetu anaumwa amepata ugonjwa wa utata hospitali zote
umeshindikana hivyo tumeenda kwa mganga wa jadi amenipa dawa na ina masharti,
inatakiwa atakaye iandaa hii dawa awe mwanamke mwenye ndoa ambaye hajawahi
kutoka nje ya ndoa tangu alipoolewa ndo kijana wetu atapona! Kama ametoka nje
ya ndoa asiandae dawa hii kwa sababu tukimpa kijana wetu watakufa wote!
Je, kina mama nani
ataandaa? Walitoka nje wamama mmoja mmoja hadi mkewe na mamake mzazi wakatoka,
akafata mama ake kijana, mashangazi na dada zake, mwisho wakabakia wanaume peke
yao! Mzee akamwambia mwanangu umeona hali za ndoa zilivyo? Acha kujisumbua
tulia na mkeo nadhani umejionea hali halisi. Cha zaidi omba Mungu sana juu ya
ndoa yako! Kijana akazimia!
Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies
WhatsApp +255 715 758 021
Post a Comment