Sehemu Ya (151) : My Dear Lovely Sisters.. Kama Upo Kwenye Mahusiano Nna Ushauri Kwa Ajili Yenu Hapa... Unaeza Jifunza Kitu.

HUWEZI KUPENDWA BILA KUJIPENDA.
Huwezi kuwa unatembea ukiwa unakula barabarani mihogo kwenye gazeti, kachori kwenye mfuko, chips kwenye foil, au miguu ya kuku na utumbo kwenye mifuko, alafu ukategemea kuheshimiwa na mwanaume anaejitambua wakati wewe hujiheshimu, jiheshimu uweshimiwe.

Usipende kuongea kwa makelele kama chiriku au kasuku ukiwa na rafiki zako alafu ukategemea kupewa siri na mpenzi au mume wako, linda kinywa chako na uropokaji ili ufaidi kushirikishwa siri za mumeo.

Acha kuchezea afya yako kwa kuboost makalio, matiti manukato kupindukia sehemu za siri na maeneo mengine kwa kigezo cha kuvutia wanaume, asilimia kubwa ya watu wanaokufa kwa magonjwa ya saratani ni wanawake, nakupa pole sana wewe unayefanya hivyo, mwanaume atakupenda jinsi ulivyo acha kumtoa Mungu kasoro kwa jinsi alivyokuumba na kujiumba mwenyewe. Ridhika na uzuri wa asili kutoka kwa Mungu, utapendwa tu.

Kupoteza muda wako kwenye mitandao kutafuta umbea huko ni kutothamini muda wako, mtu anayeshindwa kuthamini muda wake huwa ni ngumu sana kujithamini yeye binafsi. Fid q anakwambia "thamini huu muda  kabla haujageuka histori". Jikite kwenye mambo yenye tija kwako, panua akili yako kuwaza mambo yenye faida juu ya maisha yako. Usikubali kuendeshwa na mitandao dada angu.

Usipende kujiingiza kwenye mahusiano mapya mapema  kila mnapoachana na watu wako wa awali, some times yakupasa uupumzishe mwili wako na mikiki mikiki ya wanaume, pumzisha akili kutafakari aina ya mahusiano unayoitaji. Jipe thamani acha kuendeshwa na mapenzi.

Kuzaa mtoto mmoja au wawili isikufanye uchuje kiasi kwamba mwenekano wako wa awali wote unapotea, kutwa nzima unashinda na dira na mavitenge  tangu umeamka, eti ukiulizwa nini tatizo mbona unefubaa hivyo, kisingizio kisiwe kulea. Kuna watu wanawatoto zaidi ya wanne na bado wana good looking kwann wewe?. Acha kujizeesha ungali binti.


Jiheshimu ueshimike, bila kujipenda hutopendwa bali utachezewa. Wewe ni wa thamani sana kuliko unavyodhani. Badilika.

Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Ili Kupata Posts Zangu Kirahisi Zaidi Kwenye Simu Yako.http://www62.zippyshare.com/d/FvrvpQQg/31722/xxlbongotz.apk
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments