Sehemu Ya (131) : Yaani Ukiona Unajiandaa Saana Valentine's Day.. Kaa Ukijua Uhusiano Wako Una "Ufa".

Taratibu tutaelewana  tu.. Unasubiria jumatano ya tarehe 14 kwa nguvu sana ILI
IWAJE? Labda kama ni Anniversary ya penzi lenu (mlikutana siku ya tarehe hiyo) kwamba ni muhimu kuadhimisha.. Wewe penzi lako na mchuchu mmeanza june 12 valentine inawahusu nini?

Mwaka mzima ulikua wapi? Watu wenye mapenzi STRONG SIKU HII YA JUMATANO NI YA KAWAIDA SANA na wataenda skylight tu thai village kama hamna kinachoendelea , ila WEWE na uhusiano wako wa Bagia na Chumvi ndo unataka ufufukie jumatano  alafu jumapili mzike tena mpaka mwakani. Kwangu mimi Valentine ni kila siku.. Nikikuta nguo nzuri ya bebe nanunua nampelekea , hata kama ni november 19 Nikimmiss namfuata gheto tunaenda Dinner cape town fish market kula.. akiona kiatu kizuri ana nunua anani suprise , hata kama ni August 7..


Penzi lililokufa halitabustiwa na Valentine's day kamwe.. kama hupendwi hupendwi tu , penzi halifufuki jumatano huo ni mkwara nje ya net.. penzi lililojengwa kwenye misingi imara huenjoy Valentine kila siku narudia tena , ukiona umepania sana jumatano ujue penzi  lako lina shida kwasababu hata hata LEO inaweza kuwa Valentine yako ukiamua. PENZI LA KWELI HALINA TAREHE KAMA KALENDA.

Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Ili Kupata Posts Zangu Kirahisi Zaidi Kwenye Simu Yako.http://www62.zippyshare.com/d/FvrvpQQg/31722/xxlbongotz.apk
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments