Sehemu Ya (78) : Jinsi Wanawake Sikuhizi Wanavoigiza "U-Wife Material" Katika Kusaka "PETE".

Umeshawahi kujiuliza kwanini watu enzi za Uchumba walikuwa wanaonekana
wameshibana.. wanapendana... yaani ukiwatazama unaona YEESS, Natakaa kuwa kama wale..

Walipooana ukacheza kweli ukumbini, lakini ghafla baada ya mwaka unaanza kusikia kwamba Yaliyomo Hayamo.. Ndoa hakukaliki... Mdada kabla ya Ndoa alikuwa anajifanya kupeleka Vitenge kwa 'wakwe', akifika anasalimia kwa magoti hadi chini anaburuza goti getini hadi dining, wazazi wakasema Yes.. Mwanaume nae akaona Haleluyah wife material si ndo huyu.... 

Mwanamke kaomba reserve key, unarudi home unakuta nyumba imepangwa, imedekiwa na Dettol, inanukia Lady Diana Air Freshener, Tiles za bafuni zimesuguliwa na kung'arishwa na Sabuni Maarufu kutoka BUBBLY STORES Mikocheni.. Ukitoka job unavuliwa Boxer zinalowekwa, unapewa Massage hadi unasinzia, unalishwa dinner kitandani... 

Mwenyewe ukatangaza Ndoa... Umefika Ndani Mwanamke kabadilika, hapigi goti, kiburi mtindo mmoja, Usafi sifuri, ye mwenyewe kuoga hadi asikie wageni lasivyo anashinda na kanga nyonyo wazi.. Kiburi kwa Wakwe waliompigia kura ya Veto aolewe kwa kuwa na adabu.. Ndugu wa mume...

Kwa kifupi Umeoa Mtu MWEKUNDU halafu baada ya Mwaka anakuwa wa BLUU-BAHARI, anaekti U-Wife Material kusaka PETE, akishaipata sasa ndo unaona Rangi Halisi Usiwe Kinyonga Bishosti, kama ni mchafu Muonyeshe akupende na Kikwapa chako.. Kama una kiburi Onesha ajue anaoa Bumunda... 

Sio unajifanya mtaalamu wa kufua Boxer halafu ukiolewa unasema, 'Baby siwezi kufua Jeans zako Kucha zangu zinakatika', zikatike zimekuwa StejiShoo wa Baikoko??? SHOW UR TRUE COLOURS.

Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments