Sehemu Ya (71) : Ushauri Kidogo Kwa Wale Walioko Kwenye Dimbwi La Mapenzi Na Wanapitia Mapito.

Ulimuahidi kumpenda kweli na kutunza heshima yake ndiyo maaana aliwakataa
wengine na kuwa na wewe. Ulimwambia unampenda kweli na utamjali kwa shida na raha ndiyo maana alikuamini na kukukabidhi funguo ya mwili wake
Ulimwambia kamwe huwezi kumsaliti, hakukuamini katika hilo lakini ulimthibitishia tena kwa unyenyekevu na upole akakuamini na kukuomba usije kumuumiza.

Ulimuahidi na kumwambia wewe si kama wale wengine hutamuumiza moyo, hutamtesa moyo wake ukasema wewe ni wa tofauti na wale waliomuumiza.
Umesahau yote uliyoahidi, umesahau yote uliyosema hutamfanyia, leo hii unatesa, leo hii unamtoa machozi hujali tena hisia zake, leo hii umekuwa chanzo cha yeye kukosa furaha na amani, leo hii hutaki hata kusikia tena, leo hii unaona hana maana, leo hii unamuona takataka na kuona hana sifa za kuwa na wewe.

Leo hii mtoto wa watu ushampotezea dira ya maisha yake, harafu unamkataa na kuona si kitu, unajua ni kiasi gani anaumia? Unajua ni kiasi gani anapata mateso kwa akili yako?

Mungu hawezi kukuacha pekee yako, wewe upitiaye shida hizi, Mungu hawezi kuona unapata shida hizi akakuacha, tambua kuwa chozi lako haliendi bure, na elewa kuwa malipo ya kila kitu ni hapa hapa, jipe moyo kwani kesho utasimama tena, Mungu amemwandaa mtu wa kukufuta machozi yako, Mungu amemuandaa mtu wa kurejesha furaha yako. Nmeshindwa kuwashauri wote poleni sana.

Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments