Sehemu Ya (105) : Je, Waijua Dawa Ya Wale Ladies, Wanaojikuta Wako Busy.. Unapo Wahitaji??

Nilikutanaga na mrembo miaka 3 iliyopita, nilimuonesha sana kuwa namuhitaji
yani kuonana nae tena na mengineo ambayo c lazima niongee ila kama umejaaliwa uwezo wa kuelewa utakuwa umenielewa lakini ilishindikana. Basi nikamuweka kwenye kundi la marafiki wa kupiga nae stori za hapa na pale no more coz huwezi kulazimisha kitu kisicho wezekana.

Leo asubuhi nipo sehemu ya msosi nilipo geuka nikaona mtu ana nyinyooshea mkono, nikajiuliza nani yule anataka nikakae nae! NIKAJIULIZA NIME KUWA HB KIASI ICHI?😂😂 Nikaenda ila nilihisi amenifananisha so cha kwanza niliomba anikubushe mi ni nani.. Akaniambia acha masihara kila siku tunachat?

Nikamwambia uzee huu mama tusameheane but naomba unikumbushe.. Akasema nakupigia cm nikawa nimeshajua kuwa ndio wale  wako busy wote mpo dar na wilaya moja au kitongoji kimoja ila kuonana nae povu likutoke na linaweza kukutoka na usimuone TUPANGE HUKO.
Nikamwambia ukipiga nitakujua coz uwa sifutagi number ila Kwa bahati mbaya cm yangu niliacha Kwa gari so sikuweza ikabidi aniambie tu yeye ni nani nikamkumbuka.. Nime piga nae sana stori mwisho namuaga niwahi job ananiambia jumamosi nakuja kukupa hi utakuwa home?

Nikamuangalia halafu nikamwambia hapana sinto kuwepo nitakuwa Safari coz nitatoka ijumaa jioni kuelekea Songea.Basi ukirudi niambie, nikamwambia ucjali. ila Kiukweli sina safari na sitaki tena kuonana nae labda mtaani tu kama tulivyo onana leo na kuchat haina shida. Mi ni yule yule Jana, leo na hata Kesho mungu akiniweka hai siwezi badilika so kama ulikuwa busy miaka 4 Endelea kuwa busy hivyo hivyo UONE UTAPATA FAIDA GANI.


Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Ili Kupata Posts Zangu Kirahisi Zaidi Kwenye Simu Yako.http://www62.zippyshare.com/d/FvrvpQQg/31722/xxlbongotz.apk
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments