Sehemu Ya (100) : Ladies, Kama Una Tabia Zifuatazo Usishangae Ukizeekea Kwa Mama Salma.
KUOLEWA NI NDOTO KUU YA KILA MWANAMKE ALIYEKAMILIKA ILA KAMA UNA TABIA
HIZI UTAZEEKEA NYUMBANI*
*1. Tamaa ya utajiri*
fedha na mali nyingi pasipo kutambua kuwa vitu hutafutwa, hapa wengi
hupoteza nyota zao kwa kukataa wengi wenye kipato cha kawaida na kujirahisisha
kwa wenye nazo ambao kwa bahati mbaya wengi wao sio waoaji bali ni wahuni tu na
watu wa anasa na kula bata mjini.
*2. Dharau,*
maringo, kiburi na mashauzi yaani we kila mtu akikusogelea na kujaribu
kuzungumza na wewe unaanza kumpandisha na kumshusha kisha una msonya. Wengi
huishia kukupotezea wakijua either umewadharau au tayari una mtu wako ndio
maana nyodo nyingi.
*3. Husali*
hakika lazima wahuni watapata nafasi kwako na kukuchezea mpaka uchakae
kama mtumba wa uvira. MWENYEZI MUNGU ndo anaetoa BARAKA ukimuomba hakika
atakuepushia kuingia midomon mwa dubu na fisi wanaokuwa wakikuvizia na kuja
kama MALAIKA. Atakupa ufahamu wa kuwatambua na kuwashtukia mapema.
*4. Kuvaa nguo za ajabu ajabu kama changudoa*
. Sijui ni nani aliyewaambia kuwa mkivaa hivyo mnapendeza! Unakuta
binti unavaa kama mcheza show za Casino yaani ukipita nguo yaonyesha kila kitu
ukiinama ndio balaa kabisa yaani kimini kinafunuka kila kitu nje nje kwa style
hiyo nani atakupeleka kwao?
*5. Kujipaka marangi ya ajabu ajabu usoni kama mwali wa kibembe au
kizaramo kwanza mnatutisha tu.
*6. Kupenda kujirahisisha au kujipendekeza pendekeza kwa wanaume, yani
ukiguswa kidogo tu twende.
*7. Kuwa na picha karibia 500 Facebook,bTwitter n.k halafu picha
zenyewe hazieleweki yani zimepigwa katika mavazi au mapozi ya ajabu ajabu, mara
umebinua makalio, mara tumbo, mara mdomo.
*8. Kila unachofanya basi unakimbilia kupost mfano kwenye Facebook na
kadhalika
nyinginezo hata ukienda haja basi lazima upost.
*9. Ni mtu wa maneno maneno,
yani we kila unachokiona unaongea na kuropoka ropoka tu hauna break!
mwanamke gani?
*10. Huna mawazo ya malengo, endelevu yani we kwenye kichwa chako
kumejaa umbea tu sijui leo Wema Sepetu amefanya nini? Sijui Kim, Lupita Nini...
Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies
WhatsApp +255 715 758 021
Post a Comment