Sehemu Ya (146) : Hizi Hapa Baadhi Ya Tofauti Kati Ya Wasichana na Wanawake.

Wasichana wanatafuta wanaume wenye pesa ila Wanawake wanatafuta
wanaume wanaojali na kupenda.

Wasichana hupima thamani ya wanaume wao kwa kuangalia ukubwa wa mifuko yao ila Wanawake hupima thamani ya wanaume wao kwa kuangalia kiwango cha busara na hofu ya mungu na kwa vipi wanajiheshimu mbele ya wapenzi wao.

Wasichana huvunja mahusiano kwa sabubu zisizo na mashiko ila Wanawake wana uvumilivu wakifahamu kwamba kila jambo hutokea kwa sababu.

Wasichana hufikilia kuhusu mambo yaliyopo sasa ila Wanawake hufikilia kuhusu yajayo.

Wasichana wanapenda kuwa na wanaume wengi wanaowafuata ila Wanawake wanafahamu sheria ya uhitaji (Vitu rahisi vina wateja wengi).

Wasichana wanahitaji pesa ili kununua make-ups ila Wanawake wanahitaji pesa kwa ajili ya kufanyia mipango ya maendeleo.

Wasichana huumizwa na mwanaume mmoja na kuwa na kinyongo na wanaume wote ila Wanawake wanajua kwamba wanaume wote sio sawa.

Msichana "anajifunza" ila Mwanamke "anajua"

Msichana atakupenda siku ya valentine day, ila mwanamke atakupenda siku zote milele daima.

Je wewe ni msichana au mwanamke? Na Kama Ni Mwanaume Jiulize Una Date Na Mwanamke Au Msichana??


Watumiaji Wa "Android" Unaweza Download App Yangu Hapo Chini
Ili Kupata Posts Zangu Kirahisi Zaidi Kwenye Simu Yako.http://www62.zippyshare.com/d/FvrvpQQg/31722/xxlbongotz.apk
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies 
WhatsApp +255 715 758 021

No comments