Sehemu Ya (60) : Jinsi Huruma Inavyowaponza Ladies Kwenye Mahusiano.. Siku Zoote.
Una Boyfriend, Unampenda ile mbaya, anajua unampenda na
hufurukuti,
anakusumbua kwelikweli, wewe na kisima cha machozi ni Mutual
Friends, kwa mwaka unalia mara nyingi kuliko Kikundi cha Waombolezaji wa
Kinyakyusa... Imefikia muda unahisi Moyo wako umepigwa Ganzi, ukasema Enough is
Enough...
Ukaamua kumpa Moyo Mwanaume fulani, akaupokea ule moyo kama
umetengenezwa na kioo, kwa heshima zote, na anautendea haki... Yule Kinabo
aliyekutesa kwa miaka mingi ndio anashtuka, anajirudisha rudisha na kujiweka
weka karibu kutafuta Bluetooth Network kwako, wakati wewe umepata Love of your
Life.... Usivyo na akili, kisa amekuja kwako analia unahisi fisi kageuka
beberu, eti unamwonea huruma...
Mwanaume kulia machozi feki ni rahisi kuliko
Mbuzi kutembea huku anamwaga kinyesi cha Karanga... Huruma yako itakuponza,
utampoteza Mpenzi wa Ukweli na kurudi kwa janaume feki na mwisho unakosa
vyote... Huruma mwisho Chumbe! .. Eeh Mungu wasamehe hawajui watendalo hata
Maji yana aina Maji magumu na laini ... na vivyo hivyo na kwa viumbe wako.
Pia Unaweza Nifollow:
Facebook , Instagram , Snapchat , Twitter @KissToTheLadies
WhatsApp +255 715 758 021
Enter your comment...more thanks,
ReplyDelete